![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a8/Tanzania_Lindi_location_map.svg/langsw-640px-Tanzania_Lindi_location_map.svg.png&w=640&q=50)
Mkoa wa Lindi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lindi ni jina la mji, wilaya na mkoa ulioko Kusini-Mashariki mwa Tanzania.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a8/Tanzania_Lindi_location_map.svg/640px-Tanzania_Lindi_location_map.svg.png)
Mkoa wa Lindi ni kati ya mikoa 31 iliyopo nchini Tanzania yenye postikodi namba 65000.
Umepakana na mikoa ya Pwani, Mtwara, Ruvuma na Morogoro. Upande wa mashariki hupakana na Bahari Hindi.