Mfupa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mfupa ni tishu ngumu katika mwili mwa binadamu na wanyama wenye uti wa mgongo. Mifupa inahimili ogani nyingine mwilini na kuuwezesha kusimama. Mifupa ni pia kinga kwa sehemu muhimu sana kama vile mifupa ya fuvu inakinga ubongo na ubavu wa kifua unaokinga moyo na mapafu.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/3/34/Illu_compact_spongy_bone.jpg/320px-Illu_compact_spongy_bone.jpg)