![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f2/Methane.Structural_formula.V1.svg/langsw-640px-Methane.Structural_formula.V1.svg.png&w=640&q=50)
Methani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Methani ni kampaundi ya kikemia katika kundi la hidrokaboni yenye fomula CH4 maanake molekuli yake ina atomi 1 ya kaboni na atomi 4 za hidrojeni. Huhesabiwa kati ya alkani ikiwa ni sehemu kubwa ya mchanganyiko wa kawaida ya gesi asilia. Kwa halijoto ya kawaida duniani inatokea kwa umbo la gesi isiyo na herufi wala rangi. Ina nishati nyingi ndani yake inayotumiwa kwa njia ya mitambo. Asili yake iko katika mchakato wa kuoza kwa mimea na dutu ogania kwa hiyo ni fueli kisukuu.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f2/Methane.Structural_formula.V1.svg/300px-Methane.Structural_formula.V1.svg.png)
Methani hutazamiwa kati ya gesi za kupandisha halijoto duniani kali zaidi kuliko dioksidi kabonia. Kiwango chake katika angahewa kimezidi upanda tangu upimaji ulianza.