![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/58/Methane-3D-balls.png/640px-Methane-3D-balls.png&w=640&q=50)
Hidrokaboni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Hidrokaboni ni aina mbalimbali za kampaundi ogania za kikemia zinazojengwa kwa atomi za hidrojeni na kaboni pekee.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/58/Methane-3D-balls.png/640px-Methane-3D-balls.png)
Kwa asili zinapatikana hasa katika mafuta ya petroliamu iliyotokana na mchakato wa kuoza kwa mimea na mata ogania yenye kaboni na hidrojeni nyingi. Hidrokaboni haziwezi kuingia katika mmenyuko wa kikemia na maji.
Hidrokaboni ni chanzo muhimu cha nishati kwa binadamu duniani; petroli na diseli ni mchanganyiko wa aina za hidrokaboni.