![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/22/Mergus_serrator.jpg/640px-Mergus_serrator.jpg&w=640&q=50)
Bata-bahari
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mabata-bahari ni ndege wa maji wa nusufamilia ya Merginae katika familia ya Anatidae. Mabata hawa wanaishi baharini hasa nje ya majira ya kuzaa. Wengi wana tezi za chumvi maalum ambazo zinawawezesha kuvumilia maji ya bahari. Mabata-domomeno hupenda zaidi mazingira ya mito.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Bata-bahari | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Bata-domomeno kidari-chekundu (jike) | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 11: | ||||||||||||
Funga
Mabata-bahari hula samakigamba na gegereka wa chini ya bahari. Mabata-domomeno hula samaki. Meno ya madomo yao yanawasaidia kushika mawindo. Takriban spishi zote zinatokea kanda za kaskazini mbali.