Mashariki ya Kati
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mashariki ya Kati (kwa Kiingereza Middle East) ni namna ya kutaja sehemu kubwa ya Asia ya Magharibi pamoja na Afrika ya kaskazini-mashariki, hasa Misri.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/a/ac/MapRegionMiddleEast%2BTurkey.png)
Kwa kawaida nchi zifuatazo huhesabiwa humo:
- Nchi za Bara Arabu, zikiwa pamoja na Saudia, Yemen, Oman, Falme za Kiarabu, Katar na Kuwait,
- Nchi za Shamu ya kihistoria, zikiwa pamoja na Syria, Lebanon, Israel na Palestina, Yordani
- Iraq
- Uajemi
- Uturuki
- Misri (ambayo iko upande wa Afrika isipokuwa rasi ya Sinai)
Nchi hizo zinatajwa pamoja kwa sababu zina historia ya pamoja na utamaduni wa karibu.