![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e8/Mara_Andromeda.png/640px-Mara_Andromeda.png&w=640&q=50)
Mara (kundinyota)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kwa matumizi tofauti ya jina Mara angalia hapa Mara (maana)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e8/Mara_Andromeda.png/640px-Mara_Andromeda.png)
Mara ni kundinyota linalojulikana pia kwa jina lake la kimagharibi la Andromeda[1]. Ni moja ya makundinyota yanayotambuliwa na Umoja wa Kimataifa wa Astronomia [2] Jinsi ilivyo kwenye makundinyota yote, nyota za Mara hazikai pamoja hali halisi lakini zinaonekana vile tu kutoka duniani. Hali halisi kuna umbali mkubwa kati yao. Kwa hiyo "Mara" inataja eneo la angani jinsi linavyoonekana kutoka Dunia.