Mapigano ya Adowa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mapigano ya Adowa yalitokea tarehe 1 Machi 1896 katika nyanda za juu za Tigray kati ya jeshi la Italia kwa upande mmoja na la Ethiopia kwa upande mwingine. Waethiopia walishinda na kuhakikisha uhuru wa nchi yao hivyo kufanya Ethiopia nchi ya pekee ya Afrika iliyofaulu kuzuia ukoloni[1].