![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/ea/Cellarius_Harmonia_Macrocosmica_-_Planisphaerium_Ptolemaicum.jpg/640px-Cellarius_Harmonia_Macrocosmica_-_Planisphaerium_Ptolemaicum.jpg&w=640&q=50)
Majina ya nyota
From Wikipedia, the free encyclopedia
Majina ya nyota yanapatikana kwa nyota mia kadhaa zinazoonekana vema kwa macho matupu. Majina hayo yanaweza kuwa tofauti katika tamaduni mbalimbali duniani. Katika matumizi ya kisasa ni hasa majina kutoka urithi wa Ugiriki ya Kale, Roma ya Kale na Uarabuni ndio hasa yanayoendelea kutumiwa hadi leo. Pamoja na desturi ya kutunga majina kwa nyota angavu kuna pia desturi ya kupanga nyota za anga katika kundinyota zenye majina. Kundinyota ni idadi ya nyota zinazoonekana karibu kwenye anga ya usiku.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/ea/Cellarius_Harmonia_Macrocosmica_-_Planisphaerium_Ptolemaicum.jpg/640px-Cellarius_Harmonia_Macrocosmica_-_Planisphaerium_Ptolemaicum.jpg)
Leo hii Umoja wa Kimataifa wa Astronomia (UKIA) unatumia mpangilio wa kundiyota 88 zenye majina maalumu na ndani ya kundinyota hizi ilitambua majina rasmi kwa nyota angavu zaidi. UKIA ulianza kuorodhesha majina yenye asili ya Kigiriki na Kiarabu ikaendelea kukubali pia majina kutoka urithi wa tamaduni mbalimbali. Hadi mwaka 2017 majina 313 yalitambuliwa hivyo na UKIA.[1]