Lugha za Kikushi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lugha za Kikushi ni kati ya lugha za Kiafrika-Kiasia. Zinatumika hasa katika Pembe la Afrika na nchi za jirani, kuanzia Misri na Sudan hadi Kenya na Tanzania, lakini zamani zilitumika katika maeneo makubwa kuliko leo.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/19/Cushitic_languages.SVG/350px-Cushitic_languages.SVG.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/c/c7/Afro-Asiatic_language.png/640px-Afro-Asiatic_language.png)
Jina linatokana na Kush, mtu wa Biblia anayetajwa kama babu wa makabila ya aina hiyo.
Leo lugha kubwa zaidi katika kundi hilo ni Kioromo (35,000,000), kikifuatwa na Kisomali (18,000,000). Baadhi yake zimeshakufa.