Lost
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lost ni kipindi cha Marekani kinachohusu maisha ya watu waliopata ajali ya ndege iliyokuwa inatoka mjini Sydney, Australia na kuelekea mjini Los Angeles lakini ikaangukia na kupata ajali kwenye kisiwa kilichoko Oceania. Kipindi hiki kinaonyeshwa nchini Marekani kwenye stesheni ya ABC, na pia stesheni zingine kwenye nchi kadha.
Lost | |
---|---|
![]() Nembo ya Lost | |
Aina | Maigizo, Kutisha, Aksheni |
Imeongozwa | Jack Bender Stephen Williams na wengineo |
Nchi inayotoka | Marekani |
Lugha | Kiingereza |
Ina misimu | 5 |
Ina sehemu | Oahu, Hawaii (Orodha ya sehemu) |
Utayarishaji | |
Watayarishaji wakuu |
J. J. Abrams Damon Lindelof Bryan Burk Jean Higgins Jack Bender Carlton Cuse Edward Kitsis Adam Horowitz Elizabeth Sarnoff |
Sehemu | Oahu, Hawaii |
Muda | makisio ni dk. 43 |
Urushaji wa matangazo | |
Kituo | ABC |
Inarushwa na | 22 Septemba 2002 - hadi leo |
Viungo vya nje | |
Tovuti ya utayarishaji |
Kwa ajili ya kuajiri waigizaji wengi, na kurekodi filamu mjini Oahu, Hawaii, kipindi hiki kinasemekana kuwa ni cha gharama ya juu sana kwenye historia ya filamu. Ilianzishwa na Damon Lindelof, J. J. Abrams na Jeffrey Lieber na imetayarishwa na ABC Studios, Bad Robot Productions na Grass Skirt Productions. Muziki wake umeundwa na Michael Giacchino.
Kipindi hiki kinachosifika kilivutia watazamaji milioni 16 kwenye mwaka wa kwanza. Imeshinda tuzo nyingi kama Primetime Emmy Award for Outstanding Drama Series mnamo 2005[1] na tuzo la Golden Globe Award for Best Television Series - Drama|Best Drama mnamo 2006.