Liturujia ya Kilatini ni aina ya liturujia ya Ukristo iliyoenea upande wa magharibi wa Dola la Roma ambapo ilitumika lugha ya Kilatini.

Liturujia hiyo ilistawi Ulaya magharibi na Afrika kaskazini.

Polepole liturujia ya Roma, mji mkuu wa Walatini uliotawala dola hilo, ilienea katika maeneo mengi ya Kanisa Katoliki, hasa kutokana na juhudi za makusudi za kaisari Karolo Mkuu za kuunganisha mataifa yaliyokuwa chini ya himaya yake.

Baadaye Mtaguso wa Trento ulizidi kudai Wakatoliki wa magharibi wafuate wote liturujia ya Roma, isipokuwa kama liturujia yao maalumu yaliendelea zaidi ya miaka 200.

Hivyo baadhi ya liturujia nyingine za Kilatini zimedumu mpaka leo, kama vile liturujia ya Ambrosi kandokando ya Milano (Italia), liturujia ya Kimozarabu hasa huko Toledo (Hispania), liturujia ya Braga huko Ureno na kidogo liturujia ya Lyon huko Ufaransa.

Pia baadhi ya mashirika ya kitawa yanatunza liturujia za pekee.

Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Liturujia ya Kilatini kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.