Kunguni-makasia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kunguni-makasia ni wadudu wadogo wa maji wa familia Corixidae katika oda ya chini Nepomorpha ya oda Hemiptera wanaoogelea chini ya uso wa maji kwa msaada wa miguu yao ya nyuma inayofanana na makasia. Kinyume na kunguni-maji wengine, walio mbuai, kunguni-makasia hufyonza kiowevu cha mimea. Kuna takriban spishi 500 zinazotokea duniani kote kwa ujumla katika maji matamu lakini nyingi kiasi katika maji ya chumvi kidogo au hata maji ya bahari[1].
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kunguni-makasia | ||||||||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Sigara fossarum | ||||||||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||||||||
Nusufamilia 5, jenasi 52, ?? katika Afrika ya Mashariki:
| ||||||||||||||||||||||||
Funga