![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/83/Kisumu_montage.png/640px-Kisumu_montage.png&w=640&q=50)
Kisumu
Mji nchini Kenya / From Wikipedia, the free encyclopedia
Kisumu ni mji mkubwa wa tatu wa Kenya, ukiwa na wakazi 968,909 (sensa ya mwaka 2009[1]). Pia ni mji mkubwa wa Kenya ya Magharibi na makao makuu ya kaunti ya Kisumu.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/83/Kisumu_montage.png/640px-Kisumu_montage.png)
Ukweli wa haraka Nchi, Kaunti ...
Kisumu | |
Mahali pa mji wa Kisumu katika Kenya |
|
Majiranukta: 0°6′0″S 34°45′0″E | |
Nchi | ![]() |
---|---|
Kaunti | |
Kisumu | |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 968,909 |
Funga
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/4f/Jomo_Kenyatta_Stadium.jpg/640px-Jomo_Kenyatta_Stadium.jpg)
Mji uko kando ya ziwa Viktoria Nyanza, una bandari kubwa ya nchi katika ziwa hilo. Mji na bandari vilianzishwa kwa jina la "Port Florence" mwaka 1901 wakati reli ya Uganda ilipofika huko kutoka Mombasa.
Kuna feri ziwani kutoka Kisumu kwenda Mwanza, Bukoba, Entebbe, Port Bell na Jinja.
Kiuchumi Kisumu ina viwanda kadhaa, hasa vya sukari, samaki, vitambaa, pia ya bia.
Maendeleo ya Kisumu yalikwama miaka mingi kwa sababu kwa miaka mingi Wajaluo walisimama upande wa upinzani wa kisiasa, hivyo serikali haikupeleka miradi tena katika eneo hilo.