King's African Rifles
From Wikipedia, the free encyclopedia
King's African Rifles (kifupi KAR, pia huitwa Askari Kea) ilikuwa jeshi la kikoloni la Uingereza katika Afrika ya Mashariki kati ya mwaka 1902 hadi uhuru wa mataifa ya Kiafrika. Vikosi vyake vilianzishwa Kenya na kupanuka baadaye hadi koloni kwenye maeneo ya Uganda, Tanzania, na Malawi ya leo.
Baada ya uhuru vikosi vya KAR katika kila koloni vilikuwa jeshi la nchi huru vikaendelea mwanzoni kwa majina kama Uganda Rifles, Kenya Rifles. Tanganyika Rifles na Malawi Rifles.