Keir Starmer
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sir Keir Rodney Starmer (amezaliwa 2 Septemba 1962) ni mwanasiasa na wakili wa Uingereza ambaye amehudumu kama Waziri Mkuu wa Uingereza tangu 5 Julai 2024, na amekuwa kiongozi wa 19 wa Chama cha Labour tangu mwaka 2020.[1] Pia aliwahi kuwa Kiongozi wa Upinzani kutoka 2020 hadi 2024. Tangu mwaka 2015, amekuwa Mbunge wa Holborn na St Pancras, jimbo la ndani ya London. Starmer amechaguliwa tena kama Mbunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu wa 2017 na wa 2019.