Katerina wa Genoa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Katerina wa Genoa (kwa Kiitalia Caterina Fieschi Adorno) aliishi Genova nchini Italia (5 Aprili 1447 - 15 Septemba 1510) alikuwa mjane maarufu kwa kudharau malimwengu, kufunga mara nyingi, kumpenda Mungu na kuhudumia wagonjwa na wenye shida nyingine[1].
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu tangu tarehe 23 Aprili 1737, alipotangazwa na Papa Klementi XII; kabla ya hapo aliheshimiwa kama mwenye heri kuanzia tarehe 6 Aprili 1675.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Septemba kila mwaka[2].
Anajulikana hasa kwa kitabu chake kuhusu Purgatorio, alichokiandika kutokana na mang'amuzi yake katika kuwaombea marehemu wa toharani.