![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/25/Saintgermanusofparis.jpg/640px-Saintgermanusofparis.jpg&w=640&q=50)
Jermano wa Paris
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jermano wa Paris (Autun, leo nchini Ufaransa, 496 hivi - Paris, 28 Mei 576) alikuwa mmonaki ambaye, baada ya kuwa abati wa monasteri karibu na Autun, alichaguliwa kuwa askofu wa Paris akafanya uchungaji bila kulegeza maisha magumu aliyozoea[1].
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/25/Saintgermanusofparis.jpg/320px-Saintgermanusofparis.jpg)
Venansi Fortunati alimsifu sana katika kitabu alichoandika juu yake[2].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.