Hidrati kabonia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Hidrati kabonia (pia: kabohidrati au hamirojo) ni kampaundi ya kikemia inayojengwa kwa oksijeni, hidrojeni na kaboni. Katika kemia huitwa kwa jumla kwa jina "sukari" hata kama sukari kwa lugha ya kawaida ni sehemu tu ya kabohidrati.
Hidrati kabonia ni kati ya molekyuli muhimu zinazojenga viumbehai duniani. Kazi zake ni nyingi: kwa mfano, kuhifadhi na kubeba nishati (wanga) ndani ya mwili wa wanyama na mimea au kujenga mwili kwa umbo la selulosi au chitini cha wadudu.
Umbo la msingi wa kabohidrati ni monosakaridi (Cn(H2O)n) zinazoungana kuwa aina nyingine za kabohidrati.
Aina za hidrati kabonia ni kwa mfano: