Aroni (au Harun; kwa Kiebrania: אַהֲרֹן, ′aharon; kwa Kiarabu: هارون, Hārūn, kwa Kigiriki: Ἀαρών, Aaron; alifariki juu ya Mlima Hor, leo nchini Yordani, karne ya 13 KK) alikuwa kaka wa Musa. Dada yao aliitwa Mariamu.

Thumb
Aroni
Thumb
Ibada kwa ndama wa dhahabu ilivyochorwa na Nicolas Poussin.

Walikuwa watoto wa Amram na wa shangazi yake Jokebed, wote wa kabila la Lawi, taifa la Israeli.

Ndiye aliyepakwa mafuta na Musa kuwa kuhani mkuu wa kwanza wa dini yao, na makuhani wote waliofuata walitakiwa kuwa wanaume waliotokana naye kwa kuzaliwa upande wa baba[1].

Wanae waliitwa Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Julai[2].

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.