![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/c/c3/Flag_of_France.svg/langsw-640px-Flag_of_France.svg.png&w=640&q=50)
Guyani ya Kifaransa
département ya Ufaransa / From Wikipedia, the free encyclopedia
Guyani ya Kifaransa (kwa Kifaransa: Guyane française au Guyane tu, kwa Krioli ya Guyani ya Kifaransa Lagwiyann) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa ("département d'outre-mer" au DOM) katika Amerika Kusini. Makao makuu ya Guyana ni mji wa Kayeni.
Guyane Lagwiyann | |
---|---|
![]() |
![]() |
Jina la Kifaransa | Guyane (kwa Krioli:Lagwiyann) |
Jina la kawaida | Guyani ya Kifaransa |
Mji Mkuu | Kayeni |
Eneo | 86 504 km² |
Mkuu wa Mkoa | Gabriel Serville |
Idadi ya wakazi | 301 099 |
Sensa ya mwaka | 2022 |
Wakazi kwa km² | 3.2 |
Wilaya (arrondissements) | 3 |
Ramani | ![]() |
Imepakana na Brazil na Surinam. Pwani ya Bahari ya Karibi (Atlantiki) iko upande wa kaskazini.
Eneo la Guyani ni mojawapo ya mikoa tisa ya nje zaidi (OR) ya Umoja wa Ulaya. Ni eneo pekee la bara la Ufaransa na Umoja wa Ulaya huko Amerika Kusini na eneo la mwisho la Ufaransa katika bara la Amerika.
Ilikuwa koloni la Ufaransa; sasa imekuwa sehemu kamili ya Ufaransa kisiasa na kisheria. Wakazi ni raia wa Ufaransa. Eneo lina hali ya mkoa (fr:département) na pia kanda (fr:région) katika Ufaransa. Hivyo Guyani ni sehemu ya Umoja wa Ulaya. Pesa yake ni Euro.