Gesi ya machozi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Gesi ya machozi ni silaha ya kikemia inayosababisha maumivu kwenye macho na pia kwenye njia ya pumzi. Inatumiwa kama silaha isiyoua lakini kwa viwango vikubwa inaweza kuleta madhara makubwa zaidi, hadi kusababisha kifo.
Kwenye jicho inakera neva za tezi za machozi zinazoanza kutoa machozi.
Kuna dawa mbalimbali zinazotumika kwa kutengeneza gesi ya machozi,
Gesi hiyo hutumiwa kwa kawaida na polisi kwa kutawanya umati mkubwa wa watu, kuvunja maandamano au kutuliza ghasia[1].
Hairuhusiwi kuitumia vitani maana matumizi ya gesi dhidi ya wanajeshi hukataliwa na mikataba ya kimataifa, baada ya vita ya gesi sumu wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.