Geita (mji)
From Wikipedia, the free encyclopedia
2.874783°S 32.229218°E / -2.874783; 32.229218
Geita ni mji na makao makuu ya mkoa wa Geita iliyopata halmashauri yake ya pekee mnamo mwaka 2012[1].
Mji wote huwa na eneo la kilomita za mraba 1080 na maeneo yake yalitengwa na Wilaya ya Geita.
Msimbo wa posta ni 30101. [2]
Mnamo mwaka 2015 idadi ya wakazi wa Geita mjini ilikadiriwa kuwa na watu 192,541[3] Mwaka 2022 walihesabiwa 361,671 [4].
Uchumi wa Geita na kuukua kwa mji umetegemea upatikanaji wa dhahabu katika miamba ya mazingira. Uchimbaji unatekelezwa na wachimbaji wadogo na kampuni ya AngloGold Ashanti inayoajiri watu 5,000[5].