Gabriel Zubeir Wako
From Wikipedia, the free encyclopedia
Gabriel Zubeir Wako (kwa Kiarabu: غبرايل زوبير واكو; alizaliwa Mboro, Sudan, tarehe 27 Februari 1941) ni askofu mkuu wa Kanisa Katoliki aliyechunga jimbo kuu la Khartoum, Sudan.[1]
Alipata upadirisho tarehe 21 Julai 1963, akawa askofu wa jimbo la Wau mwaka 1974, halafu askofu mkuu wa Khartoum mwaka 1981.
Gabriel Zubeir Wako aliteuliwa na Papa Yohane Paulo II kuwa kardinali-padri wa parokia ya Sant'Atanasio a Via Tiburtina' tarehe 21 Oktoba 2003.
Ni kati ya makardinali walioshiriki uchaguzi wa Papa Benedikto XVI mwaka 2005 na wa Papa Fransisko mwaka 2013.
Kardinali Zubeir Wako alinusurika kuuawa wakati wa kuadhimisha Misa ya Jumapili tarehe 10 Oktoba 2010.[2] [3]
Tarehe 10 Desemba 2016 aling'atuka na kurithiwa na Askofu Mwandamizi Michael Didi Adgum Mangoria.[4]