Udeni
nchi katika Ulaya Kaskazini / From Wikipedia, the free encyclopedia
Udeni (kwa Kideni: Kongeriget Danmark) ni ufalme wa Ulaya ya Kaskazini. Ni nchi ndogo kati ya nchi za Skandinavia.
Ukweli wa haraka
| |||||
Kaulimbiu ya taifa: hakuna | |||||
Wimbo wa taifa: Der er et yndigt land (kitaifa); Kong Christian (kifalme) | |||||
Mji mkuu | Kopenhagen 55°43′ N 12°34′ E | ||||
Mji mkubwa nchini | Kopenhagen | ||||
Lugha rasmi | Kideni1 | ||||
Serikali Mfalme Waziri Mkuu |
Ufalme wa kikatiba Frederik X Mette Frederiksen | ||||
Kuungana kwa nchi {{{established_events}}} |
mnamo 980 BK | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
43,094 km² (ya 1341) 1.6%1 | ||||
Idadi ya watu - 2016 kadirio - 2006 sensa - Msongamano wa watu |
5,707,251 (ya 113) 5,450,661 132.96/km² (ya 783) | ||||
Fedha | Kroner (DKK ) | ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
CET3 (UTC+1) CEST3 (UTC+2) | ||||
Intaneti TLD | {{{cctld}}} | ||||
Kodi ya simu | +453 | ||||
1 Habari zote za Udeni bila Faroe na Grinilandi. |
Funga
Imepakana na Ujerumani upande wa kusini na kuzungukwa na maji pande tatu zilizobaki. Kaskazini kwake iko Norwei ng'ambo ya mlango wa bahari ya Skagerak, mashariki iko Uswidi ng'ambo ya Kattegat na Oresund. Bahari ya Kaskazini iko upande wa magharibi, Baltiki inaanza kwenye visiwa vikuu vya Udeni.
Greenland na visiwa vya Faroe ni sehemu ya ufalme wa Udeni lakini zinajitawala.