![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/68/White-crowned_Robin-chat.jpg/640px-White-crowned_Robin-chat.jpg&w=640&q=50)
Kurumbiza
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kurumbiza ni ndege wa jenasi mbalimbali katika familia ya Muscicapidae. Spishi nyingine zinaitwa madende. Zamani waliainishwa katika familia ya mikesha (Turdidae). Mkia wao ni mrefu kuliko ule wa zuwanende. Wana rangi ya kijivu, nyeusi, buluu au kahawa mgongoni na spishi nyingi wana koo na kidari ya rangi ya machungwa au nyekundu. Hawa ni ndege wa misitu ya Afrika na Asia. Madume ya spishi kadhaa waimba vizuri sana (k.m. Kurumbiza wa Ulaya). Hula wadudu hasa lakini spishi nyingine hula buibui, nyungunyungu na vyura na mijusi wadogo pia, na pengine hata beri. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika mti, kichaka au tundu ya asili. Jike huyataga mayai 2-6.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kurumbiza | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Kurumbiza utosi-mweupe | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 15:
| ||||||||||||||
Funga