![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/58/Universityofnairobi.jpg/640px-Universityofnairobi.jpg&w=640&q=50)
Chuo Kikuu cha Nairobi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Chuo Kikuu cha Nairobi (UoN) ni chuo kikuu kikubwa zaidi nchini Kenya. Ingawa historia yake kama taasisi ya elimu ilianza 1956, hakikufanya kuwa chuo kikuu huria mpaka 1970 wakati Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki kiligawanywa katika vyuo vikuu huria: Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nchini Tanzania, na Chuo Kikuu cha Nairobi.
Ukweli wa haraka Kimeanzishwa, Aina ...
Chuo Kikuu cha Nairobi | |
---|---|
University of Nairobi | |
Kimeanzishwa | 1956 Royal Technical College 1961 Royal College Nairobi 1964 University College Nairobi 1970 University of Nairobi |
Aina | Public |
Chansela | Joseph Barrage Wanjui |
Wanafunzi wa shahada ya kwanza | 17,200 |
Wanafunzi wa uzamili | 4,800 |
Mahali | Nairobi, Kenya |
Kampasi | Mjini |
Affiliations | ACU |
Tovuti | www.uonbi.ac.ke |
Funga
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/58/Universityofnairobi.jpg/320px-Universityofnairobi.jpg)
Mwaka wa 2002 Chuo hiki kilikuwa na wanafunzi 22,000, na 17,200 kati yao walikuwa wakisomea shahada ya msingi na 4,800 walikuwa wakisomea shahada ya kumudu. Chuo kikuu kimezindua mipango kadhaa ya kisera na kuanzisha shahada sambamba kukabiliana na mahitaji ya elimu nchini Kenya.