Chuo Kikuu cha Marburg (kwa Kijerumani: Philipps-Universität Marburg) ilianzishwa mwaka wa 1527 na Philip I, mtemi wa Hesse. Ni kimojawapo cha vyuo vikuu vya kale zaidi vya Ujerumani. Kilianzishwa kama chuo kikuu cha Kiprotestanti miaka michache baada ya matengenezo ya Martin Luther. Sasa ni chuo kikuu cha umma cha jimbo la Hesse, bila tabia ya kidini.

Chuo Kikuu cha Marburg kina wanafunzi wapatao 23,500 na wafanyakazi 7,500. Kiko katika mji wa Marburg wenye wakazi 76,000; hivyo wanafunzi na waajiriwa wa chuo kikuu ni sehemu muhimu ya uchumi wa mji wote. Majengo ya chuo kikuu yamesambaa kote kwenye mji.

Karibu asilimia 14 za wanafunzi si Wajerumani ambayo ni asilimia kubwa zaidi ya wanafunzi wa kimataifa nchini Hesse. [1]

Picha

Wahitimu mashuhuri na kitivo

Wataalamu wa sayansi asilia

 

Wanatheolojia

Marburg ilijulikana tangu mwanzoni kama chuo kikuu kinachozingatia sayansi za jamii. Ilihifadhi umaarufu huo hasa katika falsafa na theolojia kwa muda mrefu baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia .

  • Rudolf Bultmann
  • Karl Barth
  • Andreas Leonhard Creuzer
  • Friedrich Heiler
  • Wilhelm Herrmann
  • Aegidius Hunnius
  • Andreas Hyperius
  • Otto Kaiser
  • Helmut Koester
  • Jacob Lorhard
  • Rudolf Otto
  • Johann Jakob Pfeiffer
  • Kurt Rudolph
  • Annemarie Schimmel
  • Paul Tillich
  • August Friedrich Christian Vilmar
  • Gottlieb Olpp

 

Wanafalsafa

  • Wolfgang Abendroth
  • Hannah Arendt
  • Karl Theodor Bayrhoffer
  • Ernst Cassirer
  • Hermann Cohen
  • Hans-Georg Gadamer
  • Nicolai Hartmann
  • Martin Heidegger
  • Hans Heinz Holz
  • Hans Jonas
  • Friedrich Albert Lange
  • Karl Löwith
  • Paul Natorp
  • José Ortega y Gasset
  • Isaac Rülf
  • Leo Strauss
  • Christian Wolff
  • Eduard Zeller

Tanbihi

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.