Bernadeta Soubirous
From Wikipedia, the free encyclopedia
"Bernadeta" (Marie-Bernarde) Soubirous (Lourdes, Hautes-Pyrénées, 7 Januari 1844 - Nevers, Nièvre, 16 Aprili 1879) alikuwa mtawa wa Kanisa Katoliki nchini Ufaransa.
Tarehe 14 Juni 1925 Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri[1] na tarehe 8 Desemba 1933 mwenyewe alimtangaza mtakatifu bikira.[2]
Sikukuu yake imepangwa tarehe ya kifo chake[3] au 18 Februari, siku ambapo Bikira Maria alimuahidia kumpatia heri, ingawa si katika maisha ya duniani.