![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/fe/Meister_der_Sophien-Kathedrale_von_Ohrid_001.jpg/640px-Meister_der_Sophien-Kathedrale_von_Ohrid_001.jpg&w=640&q=50)
Basil wa Caesarea
From Wikipedia, the free encyclopedia
Basili wa Kaisarea (Kaisarea wa Kapadokia, leo Kayseri, nchini Uturuki, takriban 329 – Kaisarea wa Kapadokia, 1 Januari, 379) alikuwa mmonaki, halafu askofu wa mji huo (mkoa wa Kapadokia, leo nchini Uturuki).
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/fe/Meister_der_Sophien-Kathedrale_von_Ohrid_001.jpg/640px-Meister_der_Sophien-Kathedrale_von_Ohrid_001.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/6c/Basil_of_Caesarea_icon.jpg/640px-Basil_of_Caesarea_icon.jpg)
Ni mmojawapo kati ya Mababu wa Kanisa muhimu zaidi. Ndiyo sababu anaitwa Basili Mkuu (kwa Kigiriki Βασίλειος ο Μέγας).
Kwa jinsi alivyomkazia macho Kristo na kupenda watu, alianza kuheshimiwa kama mtakatifu punde baada ya kifo chake, na mwaka 1568 Papa Pius V alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa.