![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b6/TolleLege.jpg/640px-TolleLege.jpg&w=640&q=50)
Alipius wa Thagaste
From Wikipedia, the free encyclopedia
Alipius wa Thagaste alikuwa askofu wa Tagaste (leo nchini Algeria) mwaka 394. Inasemekana ndiye wa kwanza kujenga monasteri sehemu hiyo ya Afrika.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b6/TolleLege.jpg/320px-TolleLege.jpg)
Baada ya kuwa mwanafunzi wa Augustino wa Hippo, akawa kwa muda mrefu sana rafiki yake akaungana naye katika kuongokea Kanisa Katoliki (386; Confessions 8.12.28), katika maisha ya kiroho na uchungaji, ikiwa ni pamoja na kupinga uzushi[2].
Karibu yote tunayoyajua juu yake yanatokana na kitabu cha Augustino juu ya maisha yake mwenyewe Maungamo (Confessiones).
Papa Gregori XIII alimtangaza mtakatifu mwaka 1584[3] .