![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/73/Abimelech.jpg/640px-Abimelech.jpg&w=640&q=50)
Abimeleki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Abimeleki (kwa Kiebrania אֲבִימָלֶךְ, ’Ǎḇîmeleḵ[1]) mwana wa Gideoni [2] alikuwa mfalme wa Shekemu kwa muda mfupi wakati wa Waamuzi wa Biblia[3].
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/73/Abimelech.jpg/320px-Abimelech.jpg)
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/59/Dore_DeathOfAbimelech_02.jpg/320px-Dore_DeathOfAbimelech_02.jpg)
Kadiri ya Waamuzi 9:1-5 alipata ufalme kwa kuua ndugu zake wote 70, isipokuwa Yothamu aliyenusurika. Huyo alitoa hotuba yenye mfano dhidi ya Abimeleki na watu wa Shekemu waliomuunga mkono (Waamuzi 9:7-15).
Baada ya vita mbalimbali, alijeruhiwa vibaya na mwanamke aliyemrushia kutoka juu jiwe kubwa kichwani. Hapo aliagiza msaidizi wake ammalize kwa upanga.