Justin mfiadini
From Wikipedia, the free encyclopedia
Justin (pia Yustino Shahidi; Kiing. Justin Martyr; alizaliwa Flavia Neapolis, leo Nablus, Palestina, 103 hivi - Roma, Italia, kati ya 162 na 168) alikuwa mwanafalsafa ambaye, kisha kuongokea hekima halisi katika ukweli wa Yesu, aliishika katika mwenendo wa maisha yake, aliifundisha chuoni, akieneza na kutetea Ukristo hata kwa maandishi maarufu, na hatimaye akakamilisha ushahidi wake kwa kuuawa katika dhuluma ya kaisari Marko Aureli wa Dola la Roma.

Ni kwamba, baada ya kumpatia kaisari huyo utetezi wa Wakristo, alitolewa kwa mtawala Rusticus akakiri imani mbele yake na kwa ajili hiyo aliuawa pamoja na wanafunzi wake sita (Karitoni, Karito, Evelpisto, Gerasi, Peoni na Liberiani) [1].
Hati za mateso yao zimetunzwa hadi leo[2].
Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Walutheri na Waanglikana kama mtakatifu mfiadini.
Tazama pia
Maandishi yake
- Opera Omnia katika Patrologia Graeca iliyotolewa na Migne pamoja na faharasa
- First Apology
- Second Apology
- Dialogue with Trypho Greek critical edition by Philippe Bobichon
- Dialogue with Trypho the Jew
- Martyr Justin the Philosopher and those with him at Rome Orthodox Icon and Synaxarion for 1 Juni
- Dialogus cum Tryphone Judaeo - in Greek
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.