kabila kutoka Mkoa wa Mara nchini Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia
Wangurimi (au Wangoreme) ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Mara, wilaya ya Serengeti.
Lugha yao ni Kingurimi ambayo waliweza kutambua miezi yote kumi na mbili kwa majina yake kama vile mwezi 1-Kyero kembele (Januari), 2-Itaturi (Februari), 3-Kimagha (Machi), 4-Etwigho (Aprili), 5-Kyero ghekaphere (Mei), 6-Kimagha ghekaphere (Juni), 7-Nyamapheho (Julai), 8-Ringura masaringi (Agosti), 9-Nyasahi (Septemba), 10-Kemwamu (Oktoba), 11-Rughaka (Novemba), 12-Kemwamu kemwisho (Desemba).
Inasemekana walitokea katika tambarare za hifadhi ya Krugger iliyopo Afrika Kusini mwaka 1320 hivi wakanzaa harakati za kuhama taratibu kutokana na ongezeko kubwa la wadudu aina ya mbung'o walioshambulia mifugo yao na wao wenyewe. Mwaka 1740 baadhi yao walikuwa wameishafika bonde la Ufa la Ngorongoro na baadaye mwaka 1889 wakafika hifadhi ya Serengeti kusini mashariki nyika ya Loliondo. Walishabiana na wenyeji wa nyika ya Loliondo waliotambulika kama Wasonjo ambao walishabiana kwa kila kitu mfano misamiati ya lugha husika, tamaduni na kaliba.
Ilipofika miaka 1919-1932 walianza kusumbuana na kabila la Wamasai kwa kunyang'anywa mifugo yao kila itwapo leo ikawalazimu kuanza kuhama ili wasiendelee kusumbuana na Wamasai kwa kufuata tambarare za mbuga ya Serengeti na ilipofika 1945 wakawa wamefika sehemu mbalimbali za Serengeti wakiwa ni waanzilishi wa mji wa Mugumu wakiongozwa na kiongozi wao aliyeitwa Sabayaya na mdogo wake aitwaye Ikoma; hapo waliishi vizuri huku wakijishughulisha na kilimo, ufugaji maeneo ya Mangwesi na walianza kuzaliana kwa kasi kubwa iliyopelekea kutapakaa sehemu nyingi za Serengeti.
Mwaka 1970 vita vikali kati ya Wangoreme na Wakuriya vikapamba moto maeneo ya Kibaso wakati Wakuriya walipoiba ng'ombe za mzee Mokena na inakadiriwa kuwa vita hivyo vilikuwa vibaya sana kwani takribani watu 86 waliaga Dunia kwenye vita hivyo akiwemo Mgaya-Nyamori wa Majimoto Mwita-Maro wa Kisaka na wengineo wengi.
Mwaka 1989 vita vya pili kati ya Wakuriya na Wangoreme vikapamba moto baada ya Wakuriya kuiba ng'ombe za mzee Mgaya (Nyarokweli) na Motondi waliokuwa wanaishi maeneo ya tambarare za nyika za Kemgesi: inakadiriwa watu wapatao 34 walipoteza maisha.
Wangoreme wanapatikana kwa wingi huko Iramba (Ngoreme), Majimoto, Busawe, Gantamome, Kisaka Nyiboko, Nyansurumunti, Gantamome, Busawe, Mesaga, Kenyamonta, Remung'oroli, Maburi, Gusuhi, Kemgesi, Masinki, Magange, Ring'wani, Kenyana, Nyamatoke, Mosongo, Nyamitita na Bolenga.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.