From Wikipedia, the free encyclopedia
Utamaduni wa Nok ulikuwa ustaarabu wa kale katika maeneo ya Nigeria ya sasa. Ulitokea mnamo mwaka 1000 KK na kutoweka mnamo 300 BK.
Ustaarabu huo ulitambuliwa kutokana na mabaki yake ya kiakiolojia kaskazini na katikati mwa Nigeria.
Jina linatokana na kijiji cha Nok katika Jimbo la Kaduna ambako sanamu zilitambuliwa mnamo 1968 wakati wa uchimbaji katika migodi. Ufundi na ubora wa sanaa ulionyesha hali ya utamaduni wa juu, utafiti wa ardhi ambako sanamu zilikutwa ulithibitisha ni mabaki ya siku kabla ya kuzaliwa kwa Kristo. Utafiti wa udongo ulionyesha pia sanamu zote zilizopatikana katika eneo kubwa zilifinyangwa kwa udongo wa eneo moja dogo; hivyo wachunguzi walihisi eneo hilo lilikuwa na namna ya utawala au serikali ya pamoja.
Mfumo wake wa kijamii unadhaniwa kuwa uliendelea sana kwa wakati wake. Wasanii wa Nok wanaaminiwa kuwa wazalishaji wa kwanza wa sanamu ukubwa wa maisha za terakota (udongo uliochomwa) katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Wataalamu wamependekeza kuwa watu wa Nok walikuwa watangulizi wa Wayoruba wa leo. [1] [2] Walitumia chuma katika zana za kuyeyusha na kughushi kuanzia angalau mwaka 550 KK, na labda mapema zaidi. [3] [4] [5]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.