From Wikipedia, the free encyclopedia
Upinde (kutoka kitenzi "kupinda") au uta ni mti au maada nyingine iliyopindwa ambayo ncha zake zimeunganishwa kwa kamba, ukano au ngozi isiyotanishwa na hutumiwa kwa ajili ya kurushia mishale.
Inaaminika kuwa upinde wa kale kabisa ulipatikana Holmegård nchini Denmark ukiwa na miaka 8.000.
Upinde ulitengenezwa kwa minajili ya kuwinda wanyama wenye mbio na ambao hawangefikika kwa kukimbizwa mbio au kurushiwa mawe.
Baadaye, upinde ulitumika kama zana za vita jamii zilipokuwa zikikabiliana na maadui zao. Hata hivyo teknolojia hii ya kutumia upinde kama zana za vita imepitwa na wakati kwani kuna zana nyingine zilizo na haraka na bora kuliko upinde na mshale.
Leo upinde hutumika kwa minajili ya kuwinda na katika mchezo wa archery ingawapo wachezaji wa mchezo huo hutumia upinde wenye muundo tofauti na ulioboreshwa
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.