Ulama (pia: Ulema, kutoka Kiarabu علماء ʿulamāʾ) ni namna ya kutaja wataalamu wa dini katika Uislamu.
Sehemu ya mfululizo wa makala juu ya |
Imani na ibada zake |
Umoja wa Mungu |
Waislamu muhimu |
Abu Bakr • Ali |
Maandiko na Sheria |
Qur'an • Sunnah • Hadithi |
Historia ya Uislamu |
Historia |
Tamaduni za Kiislamu |
Shule • Madrasa |
Tazama pia |
Uislamu na dini nyingine |
Mamlaka na uwezo wao ni tofauti katika jamii za Kiislamu kufuatana na mapokeo tofauti. Katika madhehebu ya Shia wana athira kubwa zaidi.
Kati ya Waislamu ulema huulizwa kuhusu uelewano wa sharia na vipengele vingine vya imani.
Neno "ulama" latokana katika lugha ya Kiarabu na hapa ni wingi wa aalim (ar. عالِم) inayomaanisha "mtu mwenye elimu, mtaalamu". Neno hili linaweza kutaja wataalamu wa kila fani lakini inamaanisha hasa wataalamu wa dini[1].
Matawi ya elimu
Kimapokeo ulema hujifunza Quran, tafsir (namna ya kuelewa Qurani), Sunnah na ahadith, shariah (kanuni za imani), fiqh (namna ya kutumia sharia) na kalam (theolojia au mafundisho kuhusu imani).
Marejeo
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.