Tasmania ni kisiwa kikubwa upande wa kusini wa Australia bara ni jimbo la Australia lenye eno la 90,758 km². Mji mkuu pia mji mkubwa kisiwani ni Hobart.

Thumb
Tasmanian Devil,alama ya mnyama wa serikali ya Tasmania
Thumb
Thumb
Thumb
Tasmania katika Australia
Thumb
Bandari ya Hobart

Wenyeji asilia

Wataalamu huamini ya kwamba Tasmania ilikuwa sehemu ya bara la Australia hadi miaka 12,000 iliyopita. Wakati ule watu wameshafika kisiwani lakini kutokea kwa mlango wa bahari kuliwatenga na wenyeji wa Australia. Hivyo walikosa mawasiliano na watu wengine wakaendelea na teknolojia isiyoendelea. Wakati wa kufika kwa Wazungu katika karne ya 17 wenyeji walikuwa na vifaa vichache vya ubao na mawe tu lakini hawakuwa na pinde na mishale, hawakuvua kwa nyavu, hawakujua mashua wala kufuga wanyama au kulima.

Historia ya kikoloni

Tasmania ilifikiwa na Mholanzi Abel Tasman mwaka 1642 na kupewa jina la "Van-Diemens-Land". Tangu 1803 Uingereza ilivamia kisiwa na kuitumia kama gereza kwa wafungwa kutoka Uingereza au Australia. Walowezi na wafugaji wa kondoo walikuja pia.

Wenyeji asilia waliuawa kwa wingi hadi kupotea kabisa. Leo kuna tu wajukuu wa wanawake wenyeji waliokamatwa na Wazungu na kuzaa nao.

Wakazi

Leo hii kuna takriban watu nusu milioni kisiwani.

Maelezo zaidi Majimbo na maeneo ya Australia ...
Funga
Makala hii kuhusu maeneo ya Australia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Tasmania kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.