Ndege wadogo wa jenasi Sylvietta, familia Macrosphenidae From Wikipedia, the free encyclopedia
Vikucha au vibubutu ni ndege wadogo ambao zamani waliainishwa katika Sylviidae, familia ya kucha wengine. Sasa wataalamu wanakubaliana kwamba labda ndege hawa ni kundi lao lenyewe pamoja na kolojojo na spishi nyingine za kucha wa Afrika. Kwa sasa hakuna uhakika kama ndege hawa wote waunda familia yao au wamo katika familia mbalimbali. Wanafanana na shoro, kuchanyika na kuchamsitu ambao zamani waliainishwa pia katika familia Sylviidae. Vikucha ni wadogo zaidi na wana mkia mfupi sana. Rangi zao ni kahawia na nyekundu, kijani au njano. Hula wadudu ambao huwatafuta ardhini au kwa mashina na matawi ya miti. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikapu kwa manyasi, tandabui na nyuzinyuzi za mimea chini ya tawi la chini la mti. Jike huyataga mayai 1-3.
Kikucha | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kikucha domo-refu | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
Spishi 9:
| ||||||||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.