From Wikipedia, the free encyclopedia
Korobindo ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Ploceidae. Kuna ndege wengine ambao wanaitwa korobindo katika familia Passeridae. Spishi hizi zinatokea Afrika tu.
Korobindo | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Korobindo paji-madoa (Sporopipes frotalis | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 5, spishi 10:
| ||||||||||||
Ndege hawa wanafanana na shomoro lakini wana mwenendo kama kwera. Wana rangi ya kahawa au kijivu juu na nyeupe chini. Hula mbegu hasa na beri na wadudu pia.
Spishi hizi hulijenga tago lao ndani ya msongo wa manyasi na pengine vijitu pia ambao umebandikiwa tawi la mti. Korobindo mpendakundi hujenga jengo kubwa la manyasi linaloweza kuwa na nafasi kwa matago zaidi ya 100. Majengo haya yapo katika miti au juu ya nguzo zilizowekwa na watu kama vile nguzo za umeme. Jike huyataga mayai 3-5.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.