Simujanja
From Wikipedia, the free encyclopedia
Simujanja ni aina ya rununu ambayo inafanya mambo mengi kuliko simu nyingine ya kawaida.[1] Zinafanya kazi kama tarakilishi, lakini hiki ni chombo kinachobebeka na kidogo cha kutosha katika mkono wa mtumiaji.


Matumizi yake ni pamoja na:
- Kutuma na kupokea barua pepe, matini mafupi, picha na jumbe za media kadhaa
- Kuorodhesha mawasiliano
- Vifanyizi vya kikokotoo, fedha, king'ora, n.k.
- Kuvinjari intaneti kwa kutumia kivinjari cha simu
- Kucheza michezo mbalimbali
- Bluetooth
- GPS
- Wi-Fi
Kwa sababu simujanja ni kama tarakilishi ndogo, zinaweza kuendeshwa kwa kutumia mifumo ya uendeshaji kama vile Apple iOS na Android - itategemea na mahitaji ya chombo chenyewe. Lakini vilevile wengine wanatumia Windows Phone au BlackBerry OS.[2]
Historia

Simu ya kwanza kuuzwa ambayo inaweza kuitwa simujanja iliitwa "Angler": ilitengenezwa na Frank Canova mwaka 1992 wakati akifanya kazi IBM.[4][5][6]
Toleo lililoimarishwa zaidi liliuzwa mwaka 1994 na kampuni ya BellSouth kwa jina la Simon Personal Communicator. Pamoja na kupia na kupokea simu, simu hii iliweza pia kutuma nukushi na barua pepe. Simu hii ilikuwa na ramani, kalenda, kitabu cha namba za simu, saa, n.k.[7]
Neno "simujanja" halikutumika hadi mwaka mmoja baada ya kutolewa kwa simu hiyo.
Tazama pia
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.