From Wikipedia, the free encyclopedia
Nguchiro-bukini ni wanyama wadogo wa Madagaska wanaoainishwa katika nusufamilia Galidiinae wa familia Eupleridae na ambao wanafanana na nguchiro wa bara la Afrika. Pamoja na fungo-bukini (nusufamilia Euplerinae) wana mhenga mmoja aliyekuwa aina ya nguchiro na aliyevuka Mlango wa Msumbiji miaka milioni 20 iliyopita[1].
Nguchiro-bukini | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Nguchiro-bukini mkia-miraba (Galidia elegans) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 4, spishi 6:
| ||||||||||||||
Wanyama hawa ni kama nguchiro wadogo. Mdogo kuliko wote ni nguchiro-bukini miraba-myembamba (g 500) na mkubwa ni nguchiro-bukini wa Grandidier (g 1500). Rangi yao ni kahawia, kahawianyekundu au kijivu na wana miraba mwilini au mkiani isipokuwa spishi mbili za jenasi Salanoia.
Wanatokea misituni lakini nguchiro-bukini miraba-myembamba na wa Grandidier huishi katika maeneo wazi. Huchimba vishimo kama kikingio na spishi kadhaa hutumia matundu katika miti pia. Hula vertebrata wadogo, kama mijusi, vyura na wagugunaji, invertebrata kama wadudu na nge na hata matunda pengine.