Polima (kutoka Kiingereza "polymer") ni molekuli ndefu iliyotengenezwa kwa kuungana pamoja vizio vingi vidogo vya kemikali.

Thumb
Molekuli ya selulosi ni polima
Thumb
Vitu vilivyotengenezwa polyethilini ya polima na polypropylene.

Jina polima linatokana na neno ambalo ni la Kigiriki cha kisayansi lililopatikana kwa kuunganisha πολύ poli ‘nyingi‘ na μέρος meros ‘sehemu, kizio‘ kwa hiyo kumaanisha "ya vizio vingi". Hii inaonyesha jinsi muundo wa polima unavyokuwa na vizio vingi vidogo vilivyounganishwa pamoja kuwa molekuli kubwa.

Mmenyuko wa kikemia unaounganisha vizio vya kemikali kuunda polima huitwa upolimishaji.

Polima asilia

Polima nyingine ni za asili na zinafanywa na viumbe. Protini zina molekuli za polipeptidi. Hizi ni polima asilia zinazounganisha vizio vya asidi amino.

Selulosi na wanga (zote mbili ni kabohidrati) pia ni polima asilia zinazounganisha vizio vya glukosi. Mpira ni mchanganyiko wa polima asilia.

Polima zinazotegnezewa

Plastiki ni polima zilizotengenezwa na mwanadamu. Nyuzi nyingi zinafanywa na polima.

Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Polima kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.