From Wikipedia, the free encyclopedia
Phalangopsidae ni familia ya wadudu wanaofanana na nyenje-ardhi (Gryllidae). Nchini Afrika Kusini huitwa “bell crickets” au nyenje kengele. Inapendekezwa kutumia jina hili angalau kwa spishi za Afrika.
Phalangopsidae | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Nyenje kengele kusi (Homoeogryllus orientalis) | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||
Nusufamilia 5:
| ||||||||||||||||||
Hii ni moja ya familia kubwa zaidi za nyenje yenye spishi zinazotofautiana sana. Kwa hivyo ni ngumu kutoa maelezo ya jumla ya mofolojia na tabia zao. Spishi nyingi huonekana kuishi katika misitu, huku idadi nzuri zikiishi katika mapango. Wadudu hao hukiakia wakati wa usiku na hula dutu za kioganiki kati ya takataka za majani au takataka nyingine katika kisa cha mapango. Wakati wa mchana hujificha kwenye mashimo. Spishi nyingi hupendelea hali ya unyevunyevu, ingawa spishi nyingine huko Australia na visiwa kadhaa vya Pasifiki huishi katika hali kavu[1].
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.