Paskali Baylon
From Wikipedia, the free encyclopedia
Paskali Baylon Yubero (Torrehermosa, Zaragoza, 16 Mei 1540 - Villarreal, Castellón, 17 Mei 1592) alikuwa bruda wa utawa wa Ndugu Wadogo nchini Hispania.

Akiwa daima mwema na mkarimu kwa wote, aliabudu daima kwa upendo mkubwa fumbo la Ekaristi takatifu. Ndiyo sababu amefanywa msimamizi wa ibada zote zinazoelekea sakramenti hiyo[1].
Alitangazwa na Papa Paulo V kuwa mwenye heri tarehe 19 Oktoba 1618, halafu na Papa Alexander VIII kuwa mtakatifu tarehe 16 Oktoba 1690.
Tazama pia
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.