From Wikipedia, the free encyclopedia
Papa Leo IX (21 Juni 1002 – 19 Aprili 1054) alikuwa Papa kuanzia tarehe 2 au 12 Februari 1049 hadi kifo chake[1]. Alitokea Alsace, leo nchini Ufaransa[2].
Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Bruno wa Eguisheim-Dagsburg[3].
Alimfuata Papa Damaso II akafuatwa na Papa Viktor II.
Akielekea Roma kwa ajili ya kutawazwa, alikutana na abati Hugo wa Cluny na kumchukua mmonaki Hildebrando ambaye akaja kuwa Papa Gregori VII[4].
Alikuwa Papa bora kutoka Ujerumani katika Karne za Kati, akijitahidi kupambana na maovu ya wakati ule[5], ingawa kutokana na utawala wake lilitokea farakano na Kanisa la Kigiriki (Farakano la mwaka 1054)[6] .
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.