Historia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Historia (kutoka Kigiriki ιστορια, historia; pia "tarehe" kutoka Kiarabu تاریخ tarih kwa maana ya "historia": pia tena "mapisi") ni somo kuhusu maisha ya binadamu na utamaduni wao wakati uliopita.

Mara nyingi neno hilo lina pia maana ya maarifa yoyote kuhusu wakati uliopita, yawe au yasiwe maarifa ya watu (kwa mfano "historia ya ulimwengu").
Historia ni hasa mfululizo wa habari za mambo yaliyotokea pamoja na sababu zake.
Binadamu anaziandika ili kuelewa maisha yake, yaani ametokea wapi, amepata mafanikio gani na matatizo gani.
Historia inatufundisha kuishi: kumbukumbu za mambo ya zamani (vita, uhuru, viongozi na mengineyo) zinatuwezesha kuendelea vizuri zaidi.
Wanahistoria wanapata maarifa yao kutoka maandishi ya zamani (hasa kwa historia andishi), kutoka fasihi simulizi na kutoka akiolojia (hasa kwa historia ya awali).
Kurasa zinazohusiana
- Historia ya Afrika[1]
- Historia ya Amerika
- Historia ya Asia
- Historia ya Australia
- Historia ya Ulaya
- Historia ya Wokovu
- Historia ya Kanisa
- Historia ya teolojia
- Historia ya utawa
- Historia ya Kanisa Katoliki
- Historia ya Uislamu
- Miaka
- Vita
Tanbihi
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.