From Wikipedia, the free encyclopedia
Kuzumburu au pasa ni ndege wa familia Coliidae. Spishi zote zinatokea Afrika chini ya Sahara. Ndege hawa ni wadogo kadiri na wana mkia mrefu na kishungi kichwani. Rangi yao ni kijivu au kahawia. Huenda kwa makundi matawini kwa miti wakitafuta majani, maua na matunda ya kulika. Mwenendo huu unafanana ule wa panya na kwa sababu hiyo waitwa “mousebirds” (ndege-panya) kwa Kiingereza na majina yanayofanana kwa lugha nyingine. Kuzumburu hujenga matago kwa vitawi yenye umbo wa kikombe ambayo yamefunikwa ndani kwa manyasi. Jike huyataga mayai 2-4 na kinda huondoka tago baada ya muda mfupi tu.
Kuzumburu | ||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kuzumburu michirizi | ||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||
| ||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||
Jenasi 2 na spishi 6: | ||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.