From Wikipedia, the free encyclopedia
Koho ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Pandion, jenasi pekee ya familia Pandionidae. Zamani spishi moja tu ilifahamiwa, lakini bingwa kadhaa wamekupa nususpishi ya Australasia cheo cha spishi sasa[1] na IOC (Muungano wa Kimataifa wa Wataalamu wa Ndege) unaiafiki. Lakini wataalamu wengine hawakubali.
Koho | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Koho aliyekamata samaki | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Mwili wa koho ana sm 50-66 na upana wa mabawa ni sm 127-180. Mgongo wake una rangi ya kahawa na kidari na tumbo ni nyeupe. Mara nyingi kidari kina michirizi kahawia. Kichwa ni cheupe chenye kinyago. Vidole vyote vina urefu sawa na vina kucha za mviringo bila mfuo kinyume na vipanga na jamaa. Kidole cha nje kinaweza kugeuzwa kuelekea nyuma, kiasi kwamba koho anaweza kushika mawindo kwa vidole viwile mbele na viwili nyuma. Hii inafaa hasa akikamata samaki wenye kuteleza. Koho hula samaki takriban pekee, lakini pengine hukamata wagugunaji, amfibia, watambaazi na ndege wengine. Hutengeneza tago lao kwa vijiti juu ya mti, mhimili ya huduma za umma au mwamba. Jike huyataga mayai 2-4.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.