From Wikipedia, the free encyclopedia
Kisu (maana yake "msu mdogo"; wingi: visu) ni kifaa cha kukata chenye bapa ambalo ni kali angalau upande moja. Kwa kawaida kuna sehemu mbili: bapa kali na shikilio. Siku hizi bapa imetengenezwa kwa metali na shikilio la ubao au plastiki.
Visu vimepatikana tangu miaka lakhi: ni kati ya vifaa vya kwanza vilivyotengenzwa na binadamu tangu zama za mawe. Chanzo kilikuwa katika mawe yaliyochongwa ili kupata kona kali kwa shughuli za kukatakata.
Katika mwendo wa zama za mawe uwezo wa binadamu uliongezeka na shoka za mkononi za awali ziliweza kutengenezwa nyembamba zaidi hadi kufikia bapa la jiwe kamili.
Tangu kupatikana kwa bronzi visu vilitengenezwa zaidi kwa metali. Leo hii visu vingi vina bapa ya feleji. Siku hizi kua pia visu vya bapa za ufinyanzi wa seramiki.
Nchi malimbali huwa na sheria zinazopiga marufuku aina kadhaa za visu. Hapo kuna kanuni kuhusu urefu wa bapa ambayo mtu anaruhusiwa kubeba. Kanuni nyingine zinakataza visu ambavyo havionyeshi bapa hadi kubonyeza sehemu ya kisu na bapa inatokea kwa ghafla.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.